Karibu Soma Biblia
Mfalme anaweza kuwa mzuri au mbaya. Akiwa mfalme mzuri anaonyesha upendo kwa watu wake, na hukumu zake ni za haki. Mfalme mbaya anafikiri juu ya maendeleo yake tu, na hana rehema kwa watu wake. Karibu kusoma toleo hili ujifunze zaidi juu ya Yesu, Mfalme wa wafalme.
Mada kuu katika toleo hili la kwanza la Riziki 2024 ni Yesu Uhai Wetu. Kama vile uhai wa kipepeo ulivyokuwa mikononi mwa mjukuu, ndivyo tunavyokumbushana kuwa uhai wetu uko mikononi mwa Yesu. Aliye na Yesu anao uzima; ambaye hana Yesu, hana huo uzima. Karibu kusoma HAPA bure.
Unatafuta nguvu mpya ya kiroho? Mwongozo huu utakusaidia kujisomea Biblia kwa mpango kila siku mwaka mzima wa 2024. Bado vinapatikana Katika maduka ya Soma Biblia, karibu usichelewe kupata nakala yako
Nikukaribishe kusoma toleo hili. Linatufundisha kuwa sisi ni zawadi ya Mungu. Makala zote zinafafanua vizuri jambo hilo. Je, unamkumbuka mtoto aliyekuwa na kikapu chenye samaki wawili na mikate mitano? Soma uk.14 uone mtoto huyu alifanya nini akawa baraka ya Mungu kwa maelfu ya watu. Usisahau michezo na katuni kuhusu Dada Rehema na wadogo zake. Karibu Soma Biblia upate nakala kwa Tsh. 500 tu.
Mada kuu katika toleo hili la nne la Riziki 2023 ni Yesu Kristo ni njia ya uzima. Kuna njia nyingi, lakini tunakumbushana kuwa kuna njia moja tu ya kumwingiza mtu katika furaha ya kweli ya milele. Kuna ukweli mmoja tu umfanyao mtu kuwa huru. Kuna namna moja tu ya maisha itakayomfikisha mtu katika uzima wa milele. Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, ndiye Njia hiyo moja.
Soma Biblia tunapenda kufanya kazi ya kuhubiri Injili kwa watoto bega kwa bega na Kanisa. Tuko tayari kuchangia ili furaha na baraka ya sikukuu ya watoto iendelee muda mrefu. Inawezekana ikiwa watoto wanapewa zawadi ya kudumu zaidi ya chakula kizuri. Kwa hiyo tunatoa ofa maalumu ya vitabu fulani vinavyowafaa watoto pamoja na walezi wao wote wanaowafundisha imani na maisha ya Kikristo. Tazama picha kuona vitabu na bei ya punguzo
Je, mahubiri ya siku ya Siku Kuu ya Watoto yanawalenga akina nani hasa? Ni kwa ajili ya wazazi wanaowalea watoto au ni kwa ajili ya watoto ambao kimsingi ndio wenye siku yao? Mada kuu ya toleo la tatu la Riziki inasema “tuwafundishe watoto wetu“. Lengo la mada hii ni kukumbushana kama familia, kanisa na jamii kuweka mkazo katika malezi ya watoto. “Na watoto wako wote watafundishwa na BWANA; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi” ( Isa 54:13). Karibu kusoma RIZIKI ONLINE BURE. BOFYA HAPA
Katika toleo hili utaweza kuelewa zaidi upendo wa Yesu kwetu sisi wanadamu. Kupitia makala ya Simulizi kwa mfano utasimuliwa jinsi Yesu alivyokasirika kuona wanafunzi wake wakiwakataza watoto wasiende kwake. Unajua Yesu alifanya nini siku hiyo? Karibu usome! Na usisahau makala nyingine, vibonzo na michezo. Yote yatakupa uelewa zaidi juu ya upendo wa Mungu kwetu.
Bonyeza hapa kupata orodha ya bei ya vitabu mbali mbali na Biblia
SOMA BIBLIA Society ni shirika la wahisani lisilo la kutengeneza faida wala kuwa na mwelekeo wa kisiasa. Lengo letu kuu ni kusambaza Injili ya Yesu Kristo kwa Kiswahili, kwa kuandaa Kanisa kupitia kuendeleza, kuzalisha na kusambaza Biblia kwa njia ya sauti, machapisho ya kuaminika juu ya Injili na vifaa vingine, vyote kwa Kiswahili. Shabaha nyingine ni kuwasaidia Wakristo kufikisha Injili kwa watu na kuwafundisha kupitia neno la Mungu – juu ya imani na maisha.
Idara ya Uchapishaji
Kama ukiwa na mswada au kutaka Soma Biblia kusambaza kitabu chako. Pia masuala ya Riziki, Twende, na Soma Biblia kwa Njia ya Mtandao
Simu: +255 787 392 951
Barua Pepe: publishingmanager.somabiblia@gmail.com
Anuani ya Posta: S.L.P. 2696, Arusha, Tanzania
Makao: Eneo la Sakina, upande wa pili wa sheli ya mafuta ya Oryx (kituo cha basi huitwa Oil Com). Fuata kibao cha Scripture Mission.
Idara ya Mauzo
Kama ukitafuta kitabu na bei yake, au kutaka kuagiza na kununua vitabu
Simu: +255 754 292 995
Baruapepe: manager.somabiblia@gmail.com
Anuani ya Posta: S.L.P. 12772, Dar es Salaam, Tanzania
Makao: Barabara ya Mwai Kibaki, Mikocheni B, upande wa pili wa Sanitas Medical Centre
Maduka yanapatikana Dar es Salaam (Mikocheni B & Mbezi Luis), Arusha, Mbeya, Mwanza, Dodoma na Iringa
Nikukaribishe kusoma toleo hili. Linatufundisha kusema hapana kwa yale yasiyo mapenzi ya Mungu. Makala zote zitatutia moyo na kutujengea ujasiri wa kusema hapana. Mfano mzuri ni Danieli na rafiki zake walivyomwambia Mfalme (tazama uk.15). Kwa vijana kuna makala muhimu sana juu ya kutunza miili yetu. Na usisahau michezo na katuni kuhusu Dada Rehema na wadogo zake. TSH. 500 TU.