Contact Us

Use the form on the right to contact us.

Or use the information below to contact our main office in Dar es Salaam or Arusha.

Main office:

P.o. box 12772 Dar Es Salaam, Tanzania

Phone: +255 786 197 412

E-mail: salesmanager.somabiblia@gmail.com

Publishing department

Postal address: P.o. Box 2696 Arusha, Tanzania

Phone: + 255 787392951

E-mail: publishing.somabiblia@gmail.com

         

123 Street Avenue, City Town, 99999

(123) 555-6789

email@address.com

 

You can set your address, phone number, email and site description in the settings tab.
Link to read me page with more information.

RIZIKI TOLEO 1/2023 - Linapatikana

Habari kutoka Soma Biblia

RIZIKI TOLEO 1/2023 - Linapatikana

Cathbert Msemo

Kila mtu ana ushuhuda


Wakristo hatuna hadithi mmoja tu, bali tunazo hadithi nyingi za matendo makuu ya Mungu. Ushuhuda wetu ni hadithi za nguvu na uwezo wa Mungu katika maisha yetu. Kila siku mpya katika maisha yetu huleta hadithi mpya za wema na neema ya Mungu. Hivyo ni sawa kusema kwamba kila mkristo ana hadithi binafsi ya kusimulia, hasa tunapokumbuka kuwa Mungu ametuita mahususi, kama watu maalum na muhimu. Hadithi ya maisha yako ni ushuhuda wa wema wa Mungu, neema yake, na msamaha wake.

Katika toleo hili la Riziki tunajadili kichwa kisemacho, “Kuishi maisha ya ushuhuda’’. Lengo ni kukumbushana kuwa kila mmoja wetu anayo hadithi ya kushuhudia. Hadithi yako kuhusu kutembea na Kristo au changamoto ulizokutana nazo maishani zinaweza kufundisha, kujenga na kubadilisha maisha ya mtu mwingine anayepita kwenye hali kama yako.

Ndani ya toleo hili la Riziki utakutana na kijana mmoja ambaye hadithi yake haisemwi sana, lakini kidogo alichotuachia kina maana kubwa sana. Kijana huyu aligundua kuwa mchumba wake ni mjamzito. Sheria ya kwao ilikuwa wazi kuwa mwanamke aliyefanya jambo kama hilo alistahili adhabu kali. Lakini kijana huyu aliazimia tofauti. Unataka kujua kilichotokea? Fungua usome!

Pia utakutana na mada mbalimbali na shuhuda zitakazokusogeza mbele katika maisha yako ya kutembea na Kri-sto. Nami nasema, “Shuhuda zako, [Bwana], nimezifanya urithi wa milele; maana ndizo changamko la moyo wangu” (Zab 119:111).

Bonyeza hapa kusoma bure - RIZIKI ONLINE