Contact Us

Use the form on the right to contact us.

Or use the information below to contact our main office in Dar es Salaam or Arusha.

Main office:

P.o. box 12772 Dar Es Salaam, Tanzania

Phone: +255 786 197 412

E-mail: salesmanager.somabiblia@gmail.com

Publishing department

Postal address: P.o. Box 2696 Arusha, Tanzania

Phone: + 255 787392951

E-mail: publishing.somabiblia@gmail.com

         

123 Street Avenue, City Town, 99999

(123) 555-6789

email@address.com

 

You can set your address, phone number, email and site description in the settings tab.
Link to read me page with more information.

P6230052.JPG

Habari kutoka Soma Biblia

RIZIKI TOLEO LA 01/2022

Cathbert Msemo

Maana ya Kwaresima

Katika toleo hili la kwanza la Riziki kwa mwaka huu 2022, tunajadili masuala ya kipindi cha Kwaresima. Kanisa na waumini wake hufanya nini, na kwa nini? Na je, njia ipi ni bora zaidi, ukitaka kutumia vema kipindi hiki cha siku 40 kabla ya Pasaka? 

Utakutana na kijana mmoja ambaye alitoa wito wa ajabu kwa wanafunzi wenzake akiwaambia, “Twendeni nasi tukafe naye” (yaani, Yesu). 

Utapata pia makala mbalimbali za kukujenga na kukuimarisha kiroho, na kukusogeza karibu na Mungu. Katika majira haya ya Kwaresima naungana na nabii Yoeli kwa maneno haya, “Rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie BWANA, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi mabaya” (Yoe 3:13).

SOMA BURE HAPA, RIZIKI

RIZIKI TOLEO LA 04/2021

Cathbert Msemo

Katika toleo hili la Riziki tunajadili kuhusu nguvu ya msalaba. Ni mahali ambapo Yesu Kristo alitundikwa yapata miaka elfu mbili iliyopita, lakini tukio lile lilisababisha mabadiliko makubwa sana katika ulimwengu. Ni tukio hili ambalo lilirudisha uhusiano wa Mungu na mwanadamu. Yeye ambaye hapo kwanza alikuwa amegombana na Baba yake wa mbinguni, sasa amerudishiwa nafasi yake kama mtoto na mrithi pamoja na Kristo.

Read More

TWENDE TOLEO LA #03/2021 'Linapatikana'

Cathbert Msemo

Katika toleo hili la Twende tutajifunza zaidi kuhusu agano letu na Mungu. Ndiyo, hata sisi tunaweza kufanya agano na Mungu. Ubatizo wa Kikristo ni agano la aina hii. Vilevile utasoma kuhusu watoto waliomwahidi Mungu jambo fulani. Kama una swali kuhusu agano, karibu kumwandikia Kaka Kalamu. Yuko tayari kujibu, mia kwa mia! Karibu kununua katika maduka ya Soma Biblia kwa Tsh. 500/= tu.

Read More

SIKUKUU YA WATOTO 2021

Cathbert Msemo

Sisi wa Soma Biblia tunapenda kufanya kazi ya kuhubiri Injili kwa watoto bega kwa bega na Kanisa. Tuko tayari kuchangia ili furaha na baraka ya sikukuu ya watoto iendelee muda mrefu. Inawezekana ikiwa watoto wanapewa zawadi ya kudumu zaidi ya chakula kizuri. Kwa hiyo tunatoa ofa maalumu ya vitabu fulani vinavyowafaa watoto pamoja na walezi wao wote wanaowafundisha imani na maisha ya Kikristo.

Read More

Twende Toleo la #2, 2021 'linapatikana'

Cathbert Msemo

Katika toleo hili tumefafanua mengi juu ya imani kukua. Kwa mfano, Joni na Jeni wanasikia habari kuhusu imani, na wanavutwa kumuuliza Rehema swali; Imani ni nini?. Mazungumzo yao na majibu ya Rehema ni katika katuni. Pia kuna michezo ya kuvutia. Usisahau kututumia majibu yako kama ilivyoelekezwa kwenye uk.5 na nyuma ya gazeti.

Read More

RIZIKI toleo la 02/2021 'Usitutie majaribuni, Utuokoe na yule mwovu' linapatikana

Cathbert Msemo

Ufafanuzi wa Sala ya Bwana unaendelea katika toleo hili la Riziki. Tumefikia sehemu ya nne, Usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. Mikononi mwa Mu-ngu majaribu yanaweza kuimarisha imani yetu na kutupa uzoefu kwamba Mungu ni mwaminifu na mwenye uwezo wa kutupitisha salama kiroho. Tunapopatwa na majaribu, kisha tukavuka salama, imani yetu huwa inaongezeka. Yesu anatuombea kila wakati; tulindwe na yule mwovu. Lengo la ombi hili ni kwamba, hata katikati ya majaribu, tulindwe dhidi ya hila za yule mwovu na tuvuke salama.

Ndani ya toleo hili utakutana na watu waliopita katika majaribu yaliyogusa kila eneo la maisha yao. Hata hivyo walisimama katika imani, na hatimaye walitoka wakiwa kama dhahabu safi ing’aayo. Siri yao ikoje? Soma makala za toleo hili, na ujifunze – kwa ajili ya maisha yako mwenyewe ili uweze kuwasaidia vema wanaojaribiwa!

Read More

RIZIKI toleo la 01/2021 'Utusamehe makosa yetu' linapatikana

Cathbert Msemo

Ufafanuzi wa Sala ya Bwana unaendelea katika toleo hili la Riziki. Tumefikia sehemu ya tatu, Utusamehe makosa yetu, kama sisi tunavyowasamehe waliotukosea. Msamaha ni jambo lenye nguvu sana. Tunapenda sana msamaha, lakini mara nyingi tunapotakiwa kukiri makosa yetu au kuwasamehe waliotukosea, tunaliona kuwa jambo gumu. Tunapenda kupokea msamaha lakini hatupendi kuutoa.

Read More

SIKU KWA SIKU NA MUNGU

Cathbert Msemo

Soma Biblia tuna mfululizo wa vitabu hivi: Tafakuri za Neno la Mungu 'Siku kwa Siku na Mungu'. Kila siku unapata nafasi ya kumtafakari Mungu kupitia somo la siku husika katika vitabu hivi kwa mwaka mzima. Vitabu hivi vimetolewa kama zawadi, hivyo ni bei rahisi kupata nakala. Kwa kila kitabu ni Tsh. 2000 tu.

Read More

RIZIKI TOLEO #4/2020 'Utupe leo riziki yetu'

Cathbert Msemo

Toleo hili la RIZIKI ni muendelezo wa kuangalia Sala ya Bwana, sehemu ya pili isemayo “Utupe leo riziki yetu”. Sehemu hii inatufundisha kumwendea Mungu kwa moyo wa unyenyekevu na kumtegemea, tukimwomba atupe riziki yetu ya kila siku. Tunatiwa moyo tupeleke mahitaji yetu yafahamike kwa Mungu, tukiamini kuwa tutapewa. Kwa kuomba hivi tunakubali kwamba, kila tunachohitaji kwa ajili ya maisha yetu ya leo ni zawadi kutoka kwa Mungu.

Read More

Twende Toleo la #4, 2020 linapatikana

Cathbert Msemo

Karibu kununua TWENDE kwa Tsh. 500 tu katika maduka ya Soma Biblia. Toleo hili linafafanua juu ya Uhusiano wetu na Mungu. Kwa njia ya simulizi na hadithi nzuri utaweza kuelewa juu ya jambo hili. Utakutana pia na Dada Rehema na wenzake, na kuna michezo ya kuvutia. Usisahau kututumia majibu yako kama ilivyoelekezwa kwenye uk.5 na nyuma ya gazeti.

Read More

Soma Biblia Kila Siku 2021

Cathbert Msemo

Biblia ni taa ya miguu yake aishiye na Mungu. Soma Biblia tuna zana nzuri za kusoma Neno la Mungu kila siku. Soma Biblia kila siku 2021 ni Kalenda kamili na ufafanuzi kila siku kwa somo la Biblia

Karibu kununua nakala yako mapema katika maduka yetu ya Soma Biblia ili usichelewe kuanza mpango wa kusoma Biblia mwaka 2021.

Read More

SIKU KUU YA WATOTO 2020

Cathbert Msemo

Sisi wa Soma Biblia tunapenda kufanya kazi ya kuhubiri Injili kwa watoto bega kwa bega na Kanisa. Tuko tayari kuchangia ili furaha na baraka ya sikukuu ya watoto iendelee muda mrefu. Inawezekana ikiwa watoto wanapewa zawadi ya kudumu zaidi ya chakula kizuri.

Kwa hiyo tunatoa ofa maalumu ya vitabu fulani vinavyowafaa watoto pamoja na walezi wao wote wanaowafundisha imani na maisha ya Kikristo.

Read More

RIZIKI TOLEO LA 3/2020 'SALA YA BWANA - Bwana, utufundishe kuomba'

Cathbert Msemo

Katika toleo hili la RIZIKI tunaanza na mfululizo wa makala kuhusu Sala Kuu au Sala ya Bwana. Sala hii inatufundisha kuwa sifa zote, heshima na utukufu ni kwa Mungu wetu peke yake. Kazi yetu katika maisha ya hapa duniani na hata kifoni ni kumletea Mungu utukufu kwa kila tufanyalo. Sala hii ambayo unaweza kuiomba chini ya dakika moja inatuonyesha ukuu, urefu, upana na kina cha upendo wa Mungu kwetu kupitia Yesu Kristo.

Read More

Twende toleo la 2/2020 linapatikana

Cathbert Msemo

Ninakukaribisha usome makala zote na ujifunze mambo mazuri ya kujenga imani yako. Nikuambie! Mwaka huu Rehema atatoa zawadi kwa watoto watakaojibu vizuri maswali katika uk.5 na 6. Tazama katika ukurasa wa nyuma wa gazeti jinsi unavyoweza kutuma majibu yako. Majibu yako yakiwa sahihi, una kura moja. Tarehe 31/3, 30/6, 30/9 na 31/12 Rehema atatoa kura 15, yaani, kila mara kuna washindi 15 watakaozawadiwa.

Read More

RIZIKI TOLEO LA 2, 2020 'Sifa za Kiongozi Bora'

Cathbert Msemo

Katika toleo hili la RIZIKI tunajadili namna tunavyoweza kufikia maisha kwa kuandaa viongozi walio bora kuanzia katika umri wa ujana. Nia ni kuliamsha kanisa kama taasisi muhimu na ya kuaminika katika kuandaa viongozi wenye hofu ya Mungu, wenye maadili mema, wachapa kazi na walio tayari kuacha maslahi yao kwa ajili ya wengine.

Read More