Contact Us

Use the form on the right to contact us.

Or use the information below to contact our main office in Dar es Salaam or Arusha.

Main office:

P.o. box 12772 Dar Es Salaam, Tanzania

Phone: +255 786 197 412

E-mail: salesmanager.somabiblia@gmail.com

Publishing department

Postal address: P.o. Box 2696 Arusha, Tanzania

Phone: + 255 787392951

E-mail: publishing.somabiblia@gmail.com

         

123 Street Avenue, City Town, 99999

(123) 555-6789

email@address.com

 

You can set your address, phone number, email and site description in the settings tab.
Link to read me page with more information.

P6230052.JPG

Habari kutoka Soma Biblia

Filtering by Tag: Yesu

TWENDE 2/2023 - Linapatikana

Cathbert Msemo

Katika toleo hili utaweza kuelewa zaidi upendo wa Yesu kwetu sisi wanadamu. Kupitia makala ya Simulizi kwa mfano utasimuliwa jinsi Yesu alivyokasirika kuona wanafunzi wake wakiwakataza watoto wasiende kwake. Unajua Yesu alifanya nini siku hiyo? Karibu usome! Na usisahau makala nyingine, vibonzo na michezo. Yote yatakupa uelewa zaidi juu ya upendo wa Mungu kwetu.

Bonyeza hapa kupata orodha ya bei ya vitabu mbali mbali na Biblia

Read More

TWENDE TOLEO LA #1,2022

Cathbert Msemo

Nina mashaka, nifanye nini?

Tunapoelekea sehemu ya mbali na ni mara ya kwanza kupita katika njia ile, tunakuwa makini tusipotee. Hali ya safari inakuwa na changamoto zaidi pale tunapokutana na njia zaidi ya moja. Je, tufuate njia ipi? 

Ndani yetu kunaweza kujengeka mashaka kuwa tupo karibu na kupotea. Lakini tunapopata kuelewa na kuifuata njia iliyo sahihi, tunapata tena furaha ya safari. 

Mtoto mwenzangu, jambo hili hutokea pia katika safari yetu ya imani. Wakati mwingine changamoto ikitukuta njiani, tumaini letu linapotea, na tunapata woga na wasiwasi mkubwa. Je, tufanye nini? 

Yesu anatuambia, 'Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha' (Mathayo 11:28). Yesu anaweza kutuondolea mashaka yote tuliyonayo. Unajua anafanyaje? 

Toleo hili linafafanua jinsi kuu ya kuondokana na mashaka, nayo ni kumfuata Yesu. Yeye ni Mungu pamoja nasi. Kupitia makala mbalimbali, michezo na katuni, utajifunza na kuelewa zaidi habari hii njema. 

Karibu kununua dukani Soma Biblia kwa 500/= tu.  

RIZIKI TOLEO LA 01/2022

Cathbert Msemo

Maana ya Kwaresima

Katika toleo hili la kwanza la Riziki kwa mwaka huu 2022, tunajadili masuala ya kipindi cha Kwaresima. Kanisa na waumini wake hufanya nini, na kwa nini? Na je, njia ipi ni bora zaidi, ukitaka kutumia vema kipindi hiki cha siku 40 kabla ya Pasaka? 

Utakutana na kijana mmoja ambaye alitoa wito wa ajabu kwa wanafunzi wenzake akiwaambia, “Twendeni nasi tukafe naye” (yaani, Yesu). 

Utapata pia makala mbalimbali za kukujenga na kukuimarisha kiroho, na kukusogeza karibu na Mungu. Katika majira haya ya Kwaresima naungana na nabii Yoeli kwa maneno haya, “Rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie BWANA, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi mabaya” (Yoe 3:13).

SOMA BURE HAPA, RIZIKI

RIZIKI TOLEO 4/2019 linapatikana "JE! YESU AMEPOTEA NJIA?"

Cathbert Msemo

Katika toleo hili la RIZIKI tunajadili kurudi kwa Yesu kama alivyoahidi. Lengo ni kusaidiana kama kanisa kupeana maarifa yenye uhakika juu ya kuja kwa Yesu mara ya pili. Malengo ni wazi: Kwanza, tuwe na mafundisho sahihi kuhusu kurudi kwa Yesu. Pili, tuepukane na mafundisho ya uongo kuhusu jambo hili. Na tatu, tusije tukakata tamaa kuwa Kristo harudi, kisha tukalegea katika kuitenda kazi ya Mungu. 

Read More