SOMA BIBLIA SOCIETY ni shirika la wahisani lisilo la kutengeneza faida wala kuwa na mwelekeo wa kisiasa. Lengo letu kuu ni kusambaza Injili ya Yesu Kristo kwa Kiswahili, kwa kuandaa Kanisa kupitia kuendeleza, kuzalisha na kusambaza Biblia kwa njia ya sauti, machapisho ya kuaminika juu ya Injili na vifaa vingine. Shabaha nyingine ni kuwasaidia Wakristo kufikisha Injili kwa watu na kuwafundisha kupitia neno la Mungu – juu ya imani na maisha.
HABARI KUTOKA SOMA BIBLIA
Watoto wapendwa, karibuni! Katika toleo hili la Twende, tutajifunza kuhusu wanyama katika Biblia kama njiwa, punda na kondoo. Mungu aliwatumia kufundisha imani na maisha. Utapata michezo, vibonzo, mistari ya Biblia na wimbo wa sifa. Usikose zawadi kutoka Dada Rehema!
Nunua dukani Soma Biblia kwa 1000 tu.
“Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache” (Mt 9:37). Toleo hili la RIZIKI linakukaribisha kutafakari wito wa Yesu kwa kila muumini kushiriki katika shamba la Bwana. Usisubiri wengine, bali jiandae na ujitolee kuonesha upendo wa Kristo kwa vitendo. Karibu usome!
Soma kupitia HAPA
Kila mwanadamu amepewa zawadi ya maisha, lakini si wote hujiandaa kwa safari ya uzee. Biblia inafundisha: “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana” (Mhu 12:1). Toleo hili la RIZIKI linakukaribisha kutafakari kuzeeka kwa heshima, hekima na urithi wa kiroho. Karibu usome na ujifunze zaidi!
Unaweza kusoma bure kupitia HAPA
Toleo hili la Twende linakukaribisha kusoma na kutafakari zaidi juu ya upendo wa Mungu. Mungu hawezi kutuacha. Hatuachi gizani, anatupa tumaini jipya na furaha kila wakati. Karibu tusome pamoja, ujifunze kupitia makala, vibonzo na michezo, ukumbuke maisha ni salama kwa sababu Mungu hatuachi kamwe.
Nunua dukani Soma Biblia 1000 tu.
Ni furaha kuwaletea toleo hili la pili kwa mwaka 2025. Kwa lugha rahisi kabisa ndani ya toleo hili tutajifunza zaidi juu ya kumtumikia Mungu. Mtu mmoja alisema; "Mimi na nyumba yangu tutamtumikia Mungu". Je, wewe utamtumikia nani?
Karibu kununua katika maduka ya Soma Biblia.
Ni furaha kubwa kuwaletea wasomaji wa Riziki toleo hili la pili la mwaka 2025. Ujumbe wake ni kwamba Roho Mtakatifu ndiye mwalimu wetu mkuu.
Wasiliana nasi ukipenda kupokea kwa nia ya posta. Bonyeza Hapa
Katika maisha haya watu wengi wanatumia damu ya Yesu kwa mambo mengi. Lakini je, matumizi haya yote ni sawa? Soma toleo hili lenye kichwa ‘Neema Yatosha’.
Soma Riziki hapa Bure
Nikukaribishe kusoma toleo hili kuhusu Nuru ya Ulimwengu. Makala zote zinafafanua vizuri jambo hili. Usisahau michezo pamoja na katuni. Pia katika Sala ya Vijana utajifunza jinsi unavyoweza kuwa kielelezo kwa wengine ili nao wavutwe kumfuata Yesu kama Bwana na Mwokozi wa maisha yao. Karibu tusome! Nunua dukani Soma Biblia kwa Shilingi 500 tu.
Bonyeza link kununua dukani Soma Biblia Dar es Salaam, Mbezi Luis, Arusha, Mbeya, Iringa, Mwanza
Ni sawa kabisa kuyaita majengo yetu makubwa na mazuri kanisa. Maana yake ni mahali pa kuabudia. Katika toleo hili tutaagalia maana nyingine ya Kanisa, herufi K ikiwa kubwa. Kanisa hili si jengo bali ni sisi tunaomwamini Yesu Kristo. Ndiyo maana tunasema, "Sisi ni Kanisa la Mungu".
Bonyeza link kununua dukani Soma Biblia Dar es Salaam, Mbezi Luis, Arusha, Mbeya, Iringa, Mwanza
Mada kuu katika toleo hili la nne la Riziki 2024 inasema, Katika bonde bado Mungu yupo? Ni swali ambalo ni muhimu kutafakari ili tuwatie moyo wale ambao wanapita katika hali ngumu na kukata tamaa. Ni msaada kwa wale ambao wanapita na watakaopita katika bonde la uvuli wa mauti na kuogopa kuwa hakuna tumaini tena kwa maisha ya mbele.
Mada kuu katika toleo hili la tatu la Riziki 2024 ni Mungu wa Agano. Tunakumbushana kuwa upendo wa Mungu kwa mwanadamu ni upendo wa kipekee ambao hauwezi kulinganishwa na upendo wa aina yoyote ile. Ahadi ya kwamba hatatuacha yafungamana na agano lake nasi… Nikukaribishe kusoma - Bonyeza HAPA
Katika toleo hili tutajifunza jambo la muhimu sana tunapotaka kumpendeza Mungu na wanadamu. Jambo hili ni UTII. Kutii ni pamoja na swali gumu. Je, nimtii Mungu au mwanadamu? Wewe umewahi kujiuliza hivyo? Karibu kusoma toleo hili. TSH. 500 tu.
Mada kuu katika toleo hili la pili la Riziki 2024 ni agizo la Yesu, “Enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi wangu”. Je, uko tayari kusema, “Niko hapa Bwana, nitume mimi”?
Bonyeza hapa kusoma RIZIKI ONLINE
Karibu kusoma toleo hili ujifunze zaidi juu ya Yesu rafiki yetu. Makala zote zinafafanua vizuri jambo hili. Tsh. 500 tu.
Je, unapenda kuisoma Biblia na kuwa na hamu ya kujifunza zaidi? Basi, unaalikwa kujiunga na Ushirika wa Kujifunza Biblia! Jipatie kitabu kipya kiitwacho Mafunzo ya Biblia. Injili alivyoiandika Mathayo. Kinapatikana Soma Biblia
Bonyeza HAPA kupata bei na orodha ya vitabu vingine
Mfalme anaweza kuwa mzuri au mbaya. Akiwa mfalme mzuri anaonyesha upendo kwa watu wake, na hukumu zake ni za haki. Mfalme mbaya anafikiri juu ya maendeleo yake tu, na hana rehema kwa watu wake. Karibu kusoma toleo hili ujifunze zaidi juu ya Yesu, Mfalme wa wafalme.
Mada kuu katika toleo hili la kwanza la Riziki 2024 ni Yesu Uhai Wetu. Kama vile uhai wa kipepeo ulivyokuwa mikononi mwa mjukuu, ndivyo tunavyokumbushana kuwa uhai wetu uko mikononi mwa Yesu. Aliye na Yesu anao uzima; ambaye hana Yesu, hana huo uzima. Karibu kusoma HAPA bure.
Unatafuta nguvu mpya ya kiroho? Mwongozo huu utakusaidia kujisomea Biblia kwa mpango kila siku mwaka mzima wa 2024. Bado vinapatikana Katika maduka ya Soma Biblia, karibu usichelewe kupata nakala yako
Nikukaribishe kusoma toleo hili. Linatufundisha kuwa sisi ni zawadi ya Mungu. Makala zote zinafafanua vizuri jambo hilo. Je, unamkumbuka mtoto aliyekuwa na kikapu chenye samaki wawili na mikate mitano? Soma uk.14 uone mtoto huyu alifanya nini akawa baraka ya Mungu kwa maelfu ya watu. Usisahau michezo na katuni kuhusu Dada Rehema na wadogo zake. Karibu Soma Biblia upate nakala kwa Tsh. 500 tu.
Mada kuu katika toleo hili la nne la Riziki 2023 ni Yesu Kristo ni njia ya uzima. Kuna njia nyingi, lakini tunakumbushana kuwa kuna njia moja tu ya kumwingiza mtu katika furaha ya kweli ya milele. Kuna ukweli mmoja tu umfanyao mtu kuwa huru. Kuna namna moja tu ya maisha itakayomfikisha mtu katika uzima wa milele. Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, ndiye Njia hiyo moja.
Soma Biblia tunapenda kufanya kazi ya kuhubiri Injili kwa watoto bega kwa bega na Kanisa. Tuko tayari kuchangia ili furaha na baraka ya sikukuu ya watoto iendelee muda mrefu. Inawezekana ikiwa watoto wanapewa zawadi ya kudumu zaidi ya chakula kizuri. Kwa hiyo tunatoa ofa maalumu ya vitabu fulani vinavyowafaa watoto pamoja na walezi wao wote wanaowafundisha imani na maisha ya Kikristo. Tazama picha kuona vitabu na bei ya punguzo
Je, mahubiri ya siku ya Siku Kuu ya Watoto yanawalenga akina nani hasa? Ni kwa ajili ya wazazi wanaowalea watoto au ni kwa ajili ya watoto ambao kimsingi ndio wenye siku yao? Mada kuu ya toleo la tatu la Riziki inasema “tuwafundishe watoto wetu“. Lengo la mada hii ni kukumbushana kama familia, kanisa na jamii kuweka mkazo katika malezi ya watoto. “Na watoto wako wote watafundishwa na BWANA; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi” ( Isa 54:13). Karibu kusoma RIZIKI ONLINE BURE. BOFYA HAPA
Katika toleo hili utaweza kuelewa zaidi upendo wa Yesu kwetu sisi wanadamu. Kupitia makala ya Simulizi kwa mfano utasimuliwa jinsi Yesu alivyokasirika kuona wanafunzi wake wakiwakataza watoto wasiende kwake. Unajua Yesu alifanya nini siku hiyo? Karibu usome! Na usisahau makala nyingine, vibonzo na michezo. Yote yatakupa uelewa zaidi juu ya upendo wa Mungu kwetu.
Bonyeza hapa kupata orodha ya bei ya vitabu mbali mbali na Biblia
Katika toleo la pili la gazeti la Riziki tunajadiliana kichwa kisemacho, Vijana wanaandaliwaje kabla ya ndoa? Lengo la mada hii ni kuchochea na kuamsha mjadala juu ya kuandaa vijana wanaotarajiwa kuingia katika ndoa katika misingi ile aliyoiweka Mungu ili hata ndoa zao zitakapopata mitikisiko, bado waweze kusimama katika kumtegemea Mungu.
Soma RIZIKI ONLINE HAPA
Katika toleo hili la Riziki tunajadili kichwa kisemacho, “Kuishi maisha ya ushuhuda’’. Lengo ni kukumbushana kuwa kila mmoja wetu anayo hadithi ya kushuhudia. Hadithi yako kuhusu kutembea na Kristo au changamoto ulizokutana nazo maishani zinaweza kufundisha, kujenga na kubadilisha maisha ya mtu mwingine anayepita kwenye hali kama yako.
Bonyeza hapa kusoma bure - RIZIKI ONLINE
Maombi yanamkaribisha Yesu ndani yetu. Yanatupa nafasi ya kuzungumza na Mungu kwa karibu zaidi – kama mtoto anavyoongea na baba mzazi anayempenda. Maombi yanajibiwa kwa mapenzi ya Mungu kwetu. Mungu anatupenda, na anatukaribisha tumwombe lolote tutakalo naye atatupa. Basi ukiwa na jambo lolote, nenda katika maombi umweleze Mungu naye atajibu.
Karibu usome toleo hili linalofafanua zaidi juu ya kujibiwa maombi. Linauzwa Tsh. 500 tu, katika Maduka ya Soma Biblia
Bwana Yesu Asifiwe!
Karibu kununua Twende katika maduka ya Soma Biblia.
Katika toleo hili tutajifunza juu ya Likizo na mapumziko.
Soma Biblia tuna zana nzuri za kusoma Neno la Mungu kila siku. Soma Biblia kila siku 2023 ni Kalenda kamili na ufafanuzi kila siku kwa somo la Biblia.
Karibu kununua nakala yako mapema katika maduka yetu ya Soma Biblia
Katika toleo hili tutajifunza juu ya msamaha.
TWENDE ni gazeti la Kikristo kwa Watoto na Vijana. Kupitia gazeti hili, tunataka kufundisha Watoto na vijana Injili ya uzima wa milele ndani ya Yesu Kristo. TWENDE inatolewa mara nne kwa mwaka. Bei: 500 Tsh kwa nakala moja. Karibu dukani Soma Biblia
Mawasiliano
Idara ya Mauzo
Kama ukitafuta kitabu na bei yake, au kutaka kuagiza na kununua vitabu
Simu: +255 754 292 995
Baruapepe: manager.somabiblia@gmail.com
Anuani ya Posta: S.L.P. 12772, Dar es Salaam, Tanzania
Makao: Barabara ya Mwai Kibaki, Mikocheni B, upande wa pili wa Sanitas Medical Centre. Maduka yanapatikana Dar es Salaam (Mikocheni B & Mbezi Luis), Arusha, Mbeya, Mwanza, Dodoma na Iringa
Idara ya Uchapishaji
Ukiwa na mswada au kutaka Soma Biblia kusambaza kitabu chako.
Simu: +255 787 392 951
Barua Pepe: publishingmanager.somabiblia@gmail.com
Anuani ya Posta: S.L.P. 2696, Arusha, Tanzania
Makao: Eneo la Sakina, upande wa pili wa sheli ya mafuta ya Oryx (kituo cha basi huitwa Oil Com). Fuata kibao cha Scripture Mission.
“Niliona moja ya kipeperushi chenu kikiwa chini maeneo ya stendi ya mabasi. Kimebadilisha maisha yangu.”
— Mtu Mmoja Alisema
Nikukaribishe kusoma toleo hili. Linatufundisha kusema hapana kwa yale yasiyo mapenzi ya Mungu. Makala zote zitatutia moyo na kutujengea ujasiri wa kusema hapana. Mfano mzuri ni Danieli na rafiki zake walivyomwambia Mfalme (tazama uk.15). Kwa vijana kuna makala muhimu sana juu ya kutunza miili yetu. Na usisahau michezo na katuni kuhusu Dada Rehema na wadogo zake. TSH. 500 TU.