Soma Biblia
kwa Njia ya Mtandao

Karibu Soma Biblia kwa Njia ya Mtandao
James Sabuni

Vitabu vya Soma Biblia kwa Njia ya Mtandao

Huduma hii ni kwa wote wanaotaka
kusoma vitabu vyetu kwa manufaa zaidi

Vitabu vilivyoorodheshwa katika ukurasa huu, vimeandaliwa kama kozi yenye maswali. Ukiwa mwanafunzi wetu, mwalimu yuko tayari kukushauri, kusahihisha majibu yako na kutoa maoni na maelezo zaidi kwa lengo la kupanua uelewa wako wa mambo unayoyasoma.

Wote wanaofanya vizuri watapokea cheti kinachothibitisha kwamba wamesoma na kuelewa ujumbe wa kitabu kinachohusika.

Mafunzo ni bure. Gharama ya kusoma ni bei ya kitabu tu.

Vitabu vinaweza kununuliwa madukani kwetu, kwa wasambazaji wetu nchini kote, au kwa kuviagiza kwa Soma Bibliakwa njia ya mtandao, S.L.P. 2696, Arusha.

Baada ya kujiunga na kuchagua kitabu, mwanafunzi atapokea maswali yake kwa njia ya baruapepe au Posta, kama anavyoamua yeye. Majibu atayatuma kwa ofisi yetu mjini Arusha ambapo yatasahihishwa. Halafu tutamrudishia mwanafunzi majibu yake pamoja na cheti, ikiwa amefaulu vizuri.

Ukitaka kujiunga, peleka barua yenye jina lako, anwani yako na namba ya simu kwa anwani ya hapo juu, au tuma baruapepe kwenda kwa:

njiayaposta.somabiblia@gmail.com au piga simu: +255 686 212 165

Au jaza fomu ya kujiunga hapo pembeni na kutuma.