Riziki toleo 2/2025 'Linapatikana'
Cathbert Msemo
ROHO MTAKATIFU MWALIMU WETU
Je, tunajifunza kutoka kwa nani?
Ni furaha kubwa kuwaletea wasomaji wa Riziki toleo hili la pili la mwaka 2025. Ujumbe wake ni kwamba Roho Mtakatifu ndiye mwalimu wetu mkuu.
Pengine umewahi kujiuliza jinsi Roho Mtakatifu anavyokuongoza kama mwalimu na msaidizi, kwa mfano wakati wa changamoto na majaribu? Na je, unampa nafasi ya kufanya hivyo katika maisha yako?
Makala ya mada kuu inatukumbusha jinsi tulivyo wasahaulifu wa mafundisho ya Yesu. Lakini inaonesha pia jinsi Roho Mtakatifu anavyotwaa katika yaliyo yake Yesu na kutupasha habari yake. Tunapomtegemea Mwalimu wetu, hatupotezi mwelekeo, bali tunapata nguvu mpya ya kupambana na changamoto za maisha.
Ulimwengu wa kidijitali ni mojawapo. Una ushawishi mkubwa kwetu siku hizi. Vijana wanakabiliwa na changamoto nyingi katika masuala ya mahusiano na ndoa. Hata kama tuko wengi tunaotafuta kuwasaidia, swali hujitokeza: Nani aweze kuwapa kizazi cha kidijitali kujenga ndoa imara kwenye msingi wa uaminifu na maadili ya kikristo?
Makala ya Sasa sina woga wa kifo yatoa jibu. Anaye-shuhudia anasema, ”Neno la Mungu lilianza kunifungua macho na kunipa majibu yale yote ambayo nilikuwa nimeyahangaikia kwa miaka mingi. Sasa kitabu hiki kinazungumza nami moja kwa moja.” Bila shaka sababu ni Roho Mtakatifu, mwalimu wetu!
Je, wimbo wa zamani unaweza kutusaidia hata leo? Tumechunguza Roho Mtakatifu Mungu Wetu ili kupata jibu. Wimbo huu unaonesha jinsi Roho Mtakatifu anavyohusika na yote tunayosikia ni muhimu kwa maisha yetu.
Kwa utangulizi huu mfupi nasema, Karibu kwenye Riziki!