Watoto wapendwa, karibuni! Katika toleo hili la Twende, tutajifunza kuhusu wanyama katika Biblia kama njiwa, punda na kondoo. Mungu aliwatumia kufundisha imani na maisha. Utapata michezo, vibonzo, mistari ya Biblia na wimbo wa sifa. Usikose zawadi kutoka Dada Rehema!
Nunua dukani Soma Biblia kwa 1000 tu.
Read More
“Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache” (Mt 9:37). Toleo hili la RIZIKI linakukaribisha kutafakari wito wa Yesu kwa kila muumini kushiriki katika shamba la Bwana. Usisubiri wengine, bali jiandae na ujitolee kuonesha upendo wa Kristo kwa vitendo. Karibu usome!
Soma kupitia HAPA
Read More
Kila mwanadamu amepewa zawadi ya maisha, lakini si wote hujiandaa kwa safari ya uzee. Biblia inafundisha: “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana” (Mhu 12:1). Toleo hili la RIZIKI linakukaribisha kutafakari kuzeeka kwa heshima, hekima na urithi wa kiroho. Karibu usome na ujifunze zaidi!
Unaweza kusoma bure kupitia HAPA
Read More
Toleo hili la Twende linakukaribisha kusoma na kutafakari zaidi juu ya upendo wa Mungu. Mungu hawezi kutuacha. Hatuachi gizani, anatupa tumaini jipya na furaha kila wakati. Karibu tusome pamoja, ujifunze kupitia makala, vibonzo na michezo, ukumbuke maisha ni salama kwa sababu Mungu hatuachi kamwe.
Nunua dukani Soma Biblia 1000 tu.
Read More
Ni furaha kuwaletea toleo hili la pili kwa mwaka 2025. Kwa lugha rahisi kabisa ndani ya toleo hili tutajifunza zaidi juu ya kumtumikia Mungu. Mtu mmoja alisema; "Mimi na nyumba yangu tutamtumikia Mungu". Je, wewe utamtumikia nani?
Karibu kununua katika maduka ya Soma Biblia.
Read More
Ni furaha kubwa kuwaletea wasomaji wa Riziki toleo hili la pili la mwaka 2025. Ujumbe wake ni kwamba Roho Mtakatifu ndiye mwalimu wetu mkuu.
Wasiliana nasi ukipenda kupokea kwa nia ya posta. Bonyeza Hapa
Read More
Katika maisha haya watu wengi wanatumia damu ya Yesu kwa mambo mengi. Lakini je, matumizi haya yote ni sawa? Soma toleo hili lenye kichwa ‘Neema Yatosha’.
Soma Riziki hapa Bure
Read More
Nikukaribishe kusoma toleo hili kuhusu Nuru ya Ulimwengu. Makala zote zinafafanua vizuri jambo hili. Usisahau michezo pamoja na katuni. Pia katika Sala ya Vijana utajifunza jinsi unavyoweza kuwa kielelezo kwa wengine ili nao wavutwe kumfuata Yesu kama Bwana na Mwokozi wa maisha yao. Karibu tusome! Nunua dukani Soma Biblia kwa Shilingi 500 tu.
Bonyeza link kununua dukani Soma Biblia Dar es Salaam, Mbezi Luis, Arusha, Mbeya, Iringa, Mwanza
Read More
Ni sawa kabisa kuyaita majengo yetu makubwa na mazuri kanisa. Maana yake ni mahali pa kuabudia. Katika toleo hili tutaagalia maana nyingine ya Kanisa, herufi K ikiwa kubwa. Kanisa hili si jengo bali ni sisi tunaomwamini Yesu Kristo. Ndiyo maana tunasema, "Sisi ni Kanisa la Mungu".
Bonyeza link kununua dukani Soma Biblia Dar es Salaam, Mbezi Luis, Arusha, Mbeya, Iringa, Mwanza
Read More
Mada kuu katika toleo hili la nne la Riziki 2024 inasema, Katika bonde bado Mungu yupo? Ni swali ambalo ni muhimu kutafakari ili tuwatie moyo wale ambao wanapita katika hali ngumu na kukata tamaa. Ni msaada kwa wale ambao wanapita na watakaopita katika bonde la uvuli wa mauti na kuogopa kuwa hakuna tumaini tena kwa maisha ya mbele.
Read More
Mada kuu katika toleo hili la tatu la Riziki 2024 ni Mungu wa Agano. Tunakumbushana kuwa upendo wa Mungu kwa mwanadamu ni upendo wa kipekee ambao hauwezi kulinganishwa na upendo wa aina yoyote ile. Ahadi ya kwamba hatatuacha yafungamana na agano lake nasi… Nikukaribishe kusoma - Bonyeza HAPA
Read More
Katika toleo hili tutajifunza jambo la muhimu sana tunapotaka kumpendeza Mungu na wanadamu. Jambo hili ni UTII. Kutii ni pamoja na swali gumu. Je, nimtii Mungu au mwanadamu? Wewe umewahi kujiuliza hivyo? Karibu kusoma toleo hili. TSH. 500 tu.
Read More
Mada kuu katika toleo hili la pili la Riziki 2024 ni agizo la Yesu, “Enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi wangu”. Je, uko tayari kusema, “Niko hapa Bwana, nitume mimi”?
Bonyeza hapa kusoma RIZIKI ONLINE
Read More
Karibu kusoma toleo hili ujifunze zaidi juu ya Yesu rafiki yetu. Makala zote zinafafanua vizuri jambo hili. Tsh. 500 tu.
Read More
Je, unapenda kuisoma Biblia na kuwa na hamu ya kujifunza zaidi? Basi, unaalikwa kujiunga na Ushirika wa Kujifunza Biblia! Jipatie kitabu kipya kiitwacho Mafunzo ya Biblia. Injili alivyoiandika Mathayo. Kinapatikana Soma Biblia
Bonyeza HAPA kupata bei na orodha ya vitabu vingine
Read More
Mfalme anaweza kuwa mzuri au mbaya. Akiwa mfalme mzuri anaonyesha upendo kwa watu wake, na hukumu zake ni za haki. Mfalme mbaya anafikiri juu ya maendeleo yake tu, na hana rehema kwa watu wake. Karibu kusoma toleo hili ujifunze zaidi juu ya Yesu, Mfalme wa wafalme.
Read More
Mada kuu katika toleo hili la kwanza la Riziki 2024 ni Yesu Uhai Wetu. Kama vile uhai wa kipepeo ulivyokuwa mikononi mwa mjukuu, ndivyo tunavyokumbushana kuwa uhai wetu uko mikononi mwa Yesu. Aliye na Yesu anao uzima; ambaye hana Yesu, hana huo uzima. Karibu kusoma HAPA bure.
Read More
Unatafuta nguvu mpya ya kiroho? Mwongozo huu utakusaidia kujisomea Biblia kwa mpango kila siku mwaka mzima wa 2024. Bado vinapatikana Katika maduka ya Soma Biblia, karibu usichelewe kupata nakala yako
Read More
Nikukaribishe kusoma toleo hili. Linatufundisha kuwa sisi ni zawadi ya Mungu. Makala zote zinafafanua vizuri jambo hilo. Je, unamkumbuka mtoto aliyekuwa na kikapu chenye samaki wawili na mikate mitano? Soma uk.14 uone mtoto huyu alifanya nini akawa baraka ya Mungu kwa maelfu ya watu. Usisahau michezo na katuni kuhusu Dada Rehema na wadogo zake. Karibu Soma Biblia upate nakala kwa Tsh. 500 tu.
Read More
Mada kuu katika toleo hili la nne la Riziki 2023 ni Yesu Kristo ni njia ya uzima. Kuna njia nyingi, lakini tunakumbushana kuwa kuna njia moja tu ya kumwingiza mtu katika furaha ya kweli ya milele. Kuna ukweli mmoja tu umfanyao mtu kuwa huru. Kuna namna moja tu ya maisha itakayomfikisha mtu katika uzima wa milele. Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, ndiye Njia hiyo moja.
Read More