Soma habari mpya kutoka Soma Biblia
Riziki toleo 2/2025 'Linapatikana'
Ni furaha kubwa kuwaletea wasomaji wa Riziki toleo hili la pili la mwaka 2025. Ujumbe wake ni kwamba Roho Mtakatifu ndiye mwalimu wetu mkuu.
Wasiliana nasi ukipenda kupokea kwa nia ya posta. Bonyeza Hapa
Soma Biblia Kila Siku 2023
Soma Biblia tuna zana nzuri za kusoma Neno la Mungu kila siku. Soma Biblia kila siku 2023 ni Kalenda kamili na ufafanuzi kila siku kwa somo la Biblia.
Karibu kununua nakala yako mapema katika maduka yetu ya Soma Biblia
Biblia mpya ya lugha mbili za kiswahili na kiingereza
Sasa Biblia mpya ya lugha mbili inapatikana dukani Arusha, na Ebenezer anawakaribisha kwa furaha kubwa wateja wote. Pia katika matawi mengine ya Soma Biblia, yaani Mwanza, Iringa, Mbeya na Dar es Salaam Biblia hii inapatikana. Karibu upate nakala
SIKU KWA SIKU NA MUNGU
Soma Biblia tuna mfululizo wa vitabu hivi: Tafakuri za Neno la Mungu 'Siku kwa Siku na Mungu'. Kila siku unapata nafasi ya kumtafakari Mungu kupitia somo la siku husika katika vitabu hivi kwa mwaka mzima. Vitabu hivi vimetolewa kama zawadi, hivyo ni bei rahisi kupata nakala. Kwa kila kitabu ni Tsh. 2000 tu.
TWENDE TOLEO 1, 2020 'Linapatikana'
Katika toleo hili tutajifunza juu ya sauti ya Mungu. Je, unajua Mungu anatuita, na jinsi tunavyoweza kuisikia sauti yake na kuifuata? Karibu kusoma toleo hili uelewe vizuri zaidi.
Neno la leo
Neno la Leo ni kitabu cha kubeba popote. Mistari 4 ya Biblia inatoa mwanga kila siku.