Ndoa yenye Furaha
Kitabu hiki cha kiada kinawaandaa vizuri wanandoa watarajiwa kwa kuelewa na kufanyia kazi mafundisho ya ndoa wanayopewa kanisani kabla ya kufunga ndoa. Mambo yameratibiwa kwenye vipindi sita, vyote vikiwa na mazoezi kabla na baada ya mafundisho ya kichungaji kutolewa. Kitabu hiki ni msaidizi kweli kwa kila anayefundisha na kushauri kuhusu ndoa.
Kristo Haki Yetu
Masomo 31 ya kitabu hiki ni chakula bora na cha kiroho kwa moyo wako. Utazidi kumpenda Yesu. Kitumike kwenye sala ya binafsi au ya kifamilia.
Mwongozo kwa Familia ya Kikristo no.2
Makala 12 nyingine kuhusu maisha ya familia kwa mpango wa Mungu. Matatizo mbalimbali ya vijana yanajadiliwa. Mashauri mazuri yapo.
Mwongozo kwa Familia ya Kikristo no.1
Makala 10 zenye mafunzo na maelekezo ya Biblia kuhusu maisha ya familia kwa mpango wa Mungu, k.mf. uzazi, fedha – na ndoa ya furaha!
Ufundi wa Kuamua Ugomvi katika Ndoa
Kwa nini ugomvi hutokea katika ndoa? Mwandishi anabainisha sababu na kutoa mashauri mazuri yenye uwezo wa kuifanya ndoa kuwa imara.