11. Mfalme 4
Muda wote Sauli alikuwa ndani ya Ikulu akitafakari jinsi wananchi wake walivyompokea Daudi mapokezi ambayo hata yeye tangu awe Mfalme hajawahi kupokewa hivyo...alimuangalia Daudi kwa jicho la chuki, hasira na kisasi. Daudi hakuwa amegundua chuki za mfalme Sauli juu yake. Alikuwa amesimama tu pembeni karibu na dirisha ndani ya ikulu ya Sauli akiongea na Yonathani. Mchezo huu wa Mfalme 4 unaeleza kwa undani.
9. Mfalme 2
Mungu alimpa Daudi roho hivyo alipaswa kuwa na vifaa kwa kushughulikia kazi kama mfalme, wakati Mfalme Sauli maarufu alikuwa na kitu kingine tofauti kabisa, wakati huo huo Daudi akipokea roho, Roho wa Mungu akamwondoka Sauli. Mfalme Sauli alishikwa na ugonjwa wa ajabu akawa kama mtu aliyechanganyikiwa au aliye na mapepo. Kitu gani kinaendelea? Kipindi hiki cha Mfalme 2 kinaelezea vizuri zaidi.