15. Mkuu wa Amani 4
Yesu akazaliwa! Sikiliza kipindi hiki kujua zaidi kuhusu wageni waajabu waliowatembelea Yusufu na Mariamu baada ya Yesu kuzaliwa.
Wakati wachungaji wale wa makondeni wakianza safari kufuatia ujumbe wa Malaika. Yusufu alikuwa na wakati mgumu nje ya zizi la mifugo katika Bethlehemu, mara akae chini mara ainuke atembee aende huku na kule.... alihaha jasho jembamba likimtoka. Hatimaye akasikia sauti ya mtoto mchanga akilia sana. Yesu akazaliwa! Sikiliza kipindi hiki kujua zaidi kuhusu wageni waajabu waliowatembelea Yusufu na Mariamu baada ya Yesu kuzaliwa.
14. Mkuu wa Amani 3
Yusufu na mkewe Mariamu walikuwa wanahangaika kutafuta mahali atakapozaliwa Mfalme mpya mwokozi wa ulimwengu ajaye kutimiza mpango wa Mungu.
Wakati msafara wa ngamia wa wachunguzi wanyota ukiifuata nyota, nyota inayowaongoza toka uajemi na kusimama katika mji wa Bethlehemu mahali ambapo wanategemea watamuona mfalme mpya atakayekuwa mwokozi wa ulimwengu, Yusufu na mkewe Mariamu walikuwa wanahangaika kutafuta mahali atakapozaliwa Mfalme mpya mwokozi wa ulimwengu ajaye kutimiza mpango wa Mungu.Sikiliza kipndi hicho kujua nini itatokea.
7. Agano 5
Ibrahimu anapatwa na majaribu makubwa.
Abrahamu aliumia sana kumfukuza Ishmaeli,kwani alimpenda kama mtoto wake na alimfurahia. Pia Ilikuwa aibu kubwa kumfukuza. Abrahamu hakujua kama muda si mrefu kuna kitu kingetokea na kwamba angejaribiwa zaidi kuliko alivyokuwa akihofia. Ni kuhusu Isaka ambaye ndiye aliyebakia baada ya Ishmaieli kuondoka. Sikiliza vizuri ujifunze kupitia kipindi hiki.