15. Mkuu wa Amani 4
Yesu akazaliwa! Sikiliza kipindi hiki kujua zaidi kuhusu wageni waajabu waliowatembelea Yusufu na Mariamu baada ya Yesu kuzaliwa.
Wakati wachungaji wale wa makondeni wakianza safari kufuatia ujumbe wa Malaika. Yusufu alikuwa na wakati mgumu nje ya zizi la mifugo katika Bethlehemu, mara akae chini mara ainuke atembee aende huku na kule.... alihaha jasho jembamba likimtoka. Hatimaye akasikia sauti ya mtoto mchanga akilia sana. Yesu akazaliwa! Sikiliza kipindi hiki kujua zaidi kuhusu wageni waajabu waliowatembelea Yusufu na Mariamu baada ya Yesu kuzaliwa.
14. Mkuu wa Amani 3
Yusufu na mkewe Mariamu walikuwa wanahangaika kutafuta mahali atakapozaliwa Mfalme mpya mwokozi wa ulimwengu ajaye kutimiza mpango wa Mungu.
Wakati msafara wa ngamia wa wachunguzi wanyota ukiifuata nyota, nyota inayowaongoza toka uajemi na kusimama katika mji wa Bethlehemu mahali ambapo wanategemea watamuona mfalme mpya atakayekuwa mwokozi wa ulimwengu, Yusufu na mkewe Mariamu walikuwa wanahangaika kutafuta mahali atakapozaliwa Mfalme mpya mwokozi wa ulimwengu ajaye kutimiza mpango wa Mungu.Sikiliza kipndi hicho kujua nini itatokea.
3. AGANO 1
Safari ya Abramu kwenda nchi aliyoahidiwa na Mungu. Sehemu ya kwanza
Safari ya Abramu kwenda nchi aliyoahidiwa na Mungu ilikuwa ndefu yenye misukosuko na vikwazo vingi. Ilimchukuwa miaka kadhaa kufika nchi aliyoahidiwa na Mungu. Usiku mmoja Abramu alikuwa nje ya hema lake jangwani na kundi kubwa la watu aliofuatana nao kutoka vitani wakijenga hema kufanya makazi yao hapo. Abramu alitoka kwenye vita kuwakomboa ndugu zake. Alifanikiwa lakini alipata jeraha mguuni. Sikiliza kipindi hiki ujifunze mengi kuhusu Agano.