Contact Us

Use the form on the right to contact us.

Or use the information below to contact our main office in Dar es Salaam or Arusha.

Main office:

P.o. box 12772 Dar Es Salaam, Tanzania

Phone: +255 786 197 412

E-mail: salesmanager.somabiblia@gmail.com

Publishing department

Postal address: P.o. Box 2696 Arusha, Tanzania

Phone: + 255 787392951

E-mail: publishing.somabiblia@gmail.com

         

123 Street Avenue, City Town, 99999

(123) 555-6789

email@address.com

 

You can set your address, phone number, email and site description in the settings tab.
Link to read me page with more information.

P6230052.JPG

Habari kutoka Soma Biblia

Filtering by Category: Magazeti

RIZIKI TOLEO #4/2020 'Utupe leo riziki yetu'

Cathbert Msemo

Toleo hili la RIZIKI ni muendelezo wa kuangalia Sala ya Bwana, sehemu ya pili isemayo “Utupe leo riziki yetu”. Sehemu hii inatufundisha kumwendea Mungu kwa moyo wa unyenyekevu na kumtegemea, tukimwomba atupe riziki yetu ya kila siku. Tunatiwa moyo tupeleke mahitaji yetu yafahamike kwa Mungu, tukiamini kuwa tutapewa. Kwa kuomba hivi tunakubali kwamba, kila tunachohitaji kwa ajili ya maisha yetu ya leo ni zawadi kutoka kwa Mungu.

Read More

Twende Toleo la #4, 2020 linapatikana

Cathbert Msemo

Karibu kununua TWENDE kwa Tsh. 500 tu katika maduka ya Soma Biblia. Toleo hili linafafanua juu ya Uhusiano wetu na Mungu. Kwa njia ya simulizi na hadithi nzuri utaweza kuelewa juu ya jambo hili. Utakutana pia na Dada Rehema na wenzake, na kuna michezo ya kuvutia. Usisahau kututumia majibu yako kama ilivyoelekezwa kwenye uk.5 na nyuma ya gazeti.

Read More

RIZIKI TOLEO LA 3/2020 'SALA YA BWANA - Bwana, utufundishe kuomba'

Cathbert Msemo

Katika toleo hili la RIZIKI tunaanza na mfululizo wa makala kuhusu Sala Kuu au Sala ya Bwana. Sala hii inatufundisha kuwa sifa zote, heshima na utukufu ni kwa Mungu wetu peke yake. Kazi yetu katika maisha ya hapa duniani na hata kifoni ni kumletea Mungu utukufu kwa kila tufanyalo. Sala hii ambayo unaweza kuiomba chini ya dakika moja inatuonyesha ukuu, urefu, upana na kina cha upendo wa Mungu kwetu kupitia Yesu Kristo.

Read More

Twende toleo la 2/2020 linapatikana

Cathbert Msemo

Ninakukaribisha usome makala zote na ujifunze mambo mazuri ya kujenga imani yako. Nikuambie! Mwaka huu Rehema atatoa zawadi kwa watoto watakaojibu vizuri maswali katika uk.5 na 6. Tazama katika ukurasa wa nyuma wa gazeti jinsi unavyoweza kutuma majibu yako. Majibu yako yakiwa sahihi, una kura moja. Tarehe 31/3, 30/6, 30/9 na 31/12 Rehema atatoa kura 15, yaani, kila mara kuna washindi 15 watakaozawadiwa.

Read More

RIZIKI TOLEO LA 2, 2020 'Sifa za Kiongozi Bora'

Cathbert Msemo

Katika toleo hili la RIZIKI tunajadili namna tunavyoweza kufikia maisha kwa kuandaa viongozi walio bora kuanzia katika umri wa ujana. Nia ni kuliamsha kanisa kama taasisi muhimu na ya kuaminika katika kuandaa viongozi wenye hofu ya Mungu, wenye maadili mema, wachapa kazi na walio tayari kuacha maslahi yao kwa ajili ya wengine.

Read More

RIZIKI TOLEO LA 1, 2020 'Ujenzi wa Familia Imara'

Cathbert Msemo

Katika toleo hili la RIZIKI tunaangalia mada isemayo, “Ujenzi wa familia imara”. Lengo ni kuibua na kujadili changamoto zilizopo kwenye taasisi hii muhimu ambayo mwanzilishi wake ni Mungu mwenyewe pale bustani ya Edeni. Ni wito wa kuliamsha kanisa na jamii yote, kuwa taasisi hii inapaswa kulindwa, kuimarishwa na kupiganiwa kwa nguvu zote.

Read More

RIZIKI TOLEO 4/2019 linapatikana "JE! YESU AMEPOTEA NJIA?"

Cathbert Msemo

Katika toleo hili la RIZIKI tunajadili kurudi kwa Yesu kama alivyoahidi. Lengo ni kusaidiana kama kanisa kupeana maarifa yenye uhakika juu ya kuja kwa Yesu mara ya pili. Malengo ni wazi: Kwanza, tuwe na mafundisho sahihi kuhusu kurudi kwa Yesu. Pili, tuepukane na mafundisho ya uongo kuhusu jambo hili. Na tatu, tusije tukakata tamaa kuwa Kristo harudi, kisha tukalegea katika kuitenda kazi ya Mungu. 

Read More

RIZIKI TOLEO LA 3, 2019 'TUNATAMBUAJE NAFASI YA WATOTO NA VIJANA NDANI YA KANISA?'

Cathbert Msemo

Je, wewe ni mtumishi wa Kanisa? Riziki toleo la Tatu mwaka 2019 linapatikana sasa.


Katika toleo hili la RIZIKI tunajadili namna ya kutambua nafasi ya watoto na vijana ndani ya kanisa. Nia ni kukumbushana kama kanisa umuhimu wa kuwatambua, ili tuwalee vizuri na kuwajali pamoja na vipaji walivyo navyo. 

Read More

Twende toleo no. 3, 2018 linapatikana sasa

Cathbert Msemo

Mpendwa msomaji wa Twende, uvumilivu ni tunda la Roho tunayepewa tunapomwamini Yesu. Biblia inatufundisha uvumilivu kupitia watu mbalimbali. Toleo hili limefafanua zaidi maana ya uvumilivu kwetu sisi Wakristo. Jipatie nakala yako kutoka Soma Biblia.

Read More