Toleo hili la RIZIKI ni muendelezo wa kuangalia Sala ya Bwana, sehemu ya pili isemayo “Utupe leo riziki yetu”. Sehemu hii inatufundisha kumwendea Mungu kwa moyo wa unyenyekevu na kumtegemea, tukimwomba atupe riziki yetu ya kila siku. Tunatiwa moyo tupeleke mahitaji yetu yafahamike kwa Mungu, tukiamini kuwa tutapewa. Kwa kuomba hivi tunakubali kwamba, kila tunachohitaji kwa ajili ya maisha yetu ya leo ni zawadi kutoka kwa Mungu.
Read More
Karibu kununua TWENDE kwa Tsh. 500 tu katika maduka ya Soma Biblia. Toleo hili linafafanua juu ya Uhusiano wetu na Mungu. Kwa njia ya simulizi na hadithi nzuri utaweza kuelewa juu ya jambo hili. Utakutana pia na Dada Rehema na wenzake, na kuna michezo ya kuvutia. Usisahau kututumia majibu yako kama ilivyoelekezwa kwenye uk.5 na nyuma ya gazeti.
Read More
Katika toleo hili la RIZIKI tunaanza na mfululizo wa makala kuhusu Sala Kuu au Sala ya Bwana. Sala hii inatufundisha kuwa sifa zote, heshima na utukufu ni kwa Mungu wetu peke yake. Kazi yetu katika maisha ya hapa duniani na hata kifoni ni kumletea Mungu utukufu kwa kila tufanyalo. Sala hii ambayo unaweza kuiomba chini ya dakika moja inatuonyesha ukuu, urefu, upana na kina cha upendo wa Mungu kwetu kupitia Yesu Kristo.
Read More
Katika toleo hili tumefafanua zaidi jinsi Mungu anavyotutunza.
Read More
Ninakukaribisha usome makala zote na ujifunze mambo mazuri ya kujenga imani yako. Nikuambie! Mwaka huu Rehema atatoa zawadi kwa watoto watakaojibu vizuri maswali katika uk.5 na 6. Tazama katika ukurasa wa nyuma wa gazeti jinsi unavyoweza kutuma majibu yako. Majibu yako yakiwa sahihi, una kura moja. Tarehe 31/3, 30/6, 30/9 na 31/12 Rehema atatoa kura 15, yaani, kila mara kuna washindi 15 watakaozawadiwa.
Read More
Katika toleo hili la RIZIKI tunajadili namna tunavyoweza kufikia maisha kwa kuandaa viongozi walio bora kuanzia katika umri wa ujana. Nia ni kuliamsha kanisa kama taasisi muhimu na ya kuaminika katika kuandaa viongozi wenye hofu ya Mungu, wenye maadili mema, wachapa kazi na walio tayari kuacha maslahi yao kwa ajili ya wengine.
Read More
Katika toleo hili tutajifunza juu ya sauti ya Mungu. Je, unajua Mungu anatuita, na jinsi tunavyoweza kuisikia sauti yake na kuifuata? Karibu kusoma toleo hili uelewe vizuri zaidi.
Read More
Katika toleo hili la RIZIKI tunaangalia mada isemayo, “Ujenzi wa familia imara”. Lengo ni kuibua na kujadili changamoto zilizopo kwenye taasisi hii muhimu ambayo mwanzilishi wake ni Mungu mwenyewe pale bustani ya Edeni. Ni wito wa kuliamsha kanisa na jamii yote, kuwa taasisi hii inapaswa kulindwa, kuimarishwa na kupiganiwa kwa nguvu zote.
Read More
Katika toleo hili la RIZIKI tunajadili kurudi kwa Yesu kama alivyoahidi. Lengo ni kusaidiana kama kanisa kupeana maarifa yenye uhakika juu ya kuja kwa Yesu mara ya pili. Malengo ni wazi: Kwanza, tuwe na mafundisho sahihi kuhusu kurudi kwa Yesu. Pili, tuepukane na mafundisho ya uongo kuhusu jambo hili. Na tatu, tusije tukakata tamaa kuwa Kristo harudi, kisha tukalegea katika kuitenda kazi ya Mungu.
Read More
Mtoto mwenzangu, toleo hili lina habari njema kuhusu maisha yetu ya sasa na ya baadaye. Tutambue kwamba tukiwa ndani ya Yesu tutakuwa salama sasa na siku zijazo, na hata tukifa tutaenda kuishi na Yesu kwa furaha mbinguni.
Read More
Habari hii njema tunafafanua zaidi katika toleo hili. Na wewe Kijana mpendwa, usisahau kuna makala nzuri kwa ajili yako pia. Inahusu miiba. Lakini Yesu yupo kukulinda isikuchome!
Read More
Je, wewe ni mtumishi wa Kanisa? Riziki toleo la Tatu mwaka 2019 linapatikana sasa.
Katika toleo hili la RIZIKI tunajadili namna ya kutambua nafasi ya watoto na vijana ndani ya kanisa. Nia ni kukumbushana kama kanisa umuhimu wa kuwatambua, ili tuwalee vizuri na kuwajali pamoja na vipaji walivyo navyo.
Read More
Umewahi kusikia mtu akisema, “Mimi ni mwanafunzi wa Yesu”? Au, “Mimi ni mtoto wa Yesu? Au, “Mimi ni mtumishi wa Yesu? Je, ana maana gani hasa? Soma makala za gazeti hili upate ufafanuzi mzuri kuhusu swali hili.
Read More
Katika toleo hili la Riziki tunajadili kuhusu umisioni wa ndani. Lengo ni kukumbusha juu ya Utume mkuu wa Bwana Yesu wa kwenda kuhubiri habari njema ya toba na ondoleo la dhambi kwa wale ambao hawajafikiwa na injili.
Read More
Gazeti hili maalum kwa watoto na vijana linazungumzia maana ya Amani kwa Wakristo. Amani ni usalama, raha moyoni na raha ya kutenda. Ni toleo la 4 kwa mwaka 2018 na lipo madukani Soma Biblia. Karibu umnunulie mtoto zawadi hii idumuyo na yenye kubeba mafundisho ya Neno la Mungu.
Read More
Katika toleo hili la RIZIKI tunaangalia sehemu ya tatu ya Imani ya Mitume inayoanza kwa kusema, Namwamini Roho Mtakatifu. Tunaamini yaliyomo katika toleo hili yataimarisha imani yako katika kumwamini Roho Mtakatifu.
Read More
Mpendwa msomaji wa Twende, uvumilivu ni tunda la Roho tunayepewa tunapomwamini Yesu. Biblia inatufundisha uvumilivu kupitia watu mbalimbali. Toleo hili limefafanua zaidi maana ya uvumilivu kwetu sisi Wakristo. Jipatie nakala yako kutoka Soma Biblia.
Read More
Toleo hili la RIZIKI tunaangalia sehemu ya pili ya Imani ya Mitume; Namwamini Yesu Kristo. Tunakumbushana kwa kutafakari maana ya maneno haya. Tunapokiri kwamba namwamini yesu, ina maana maisha yetu yamejengeka ndani ya msingi ambao ni Yesu Kristo.
Read More
Je, nini itatokea kwa imani yetu, ikiwa kila kizazi huibadilisha tu kulingarna na mawazo, mahitaji na mipango yake? Katika RIZIKI toleo la kwanza 2018, tutaangelia zaidi maneno muhimu kuhusu Imani yetu ya Kikristo.
Read More
Mimi na wewe tunaweza kuwa na maswali mengi yanayosumbua imani yetu kututilia wasiwasi mwingi wa kiroho.
Read More