7. Agano 5
Ibrahimu anapatwa na majaribu makubwa.
Abrahamu aliumia sana kumfukuza Ishmaeli,kwani alimpenda kama mtoto wake na alimfurahia. Pia Ilikuwa aibu kubwa kumfukuza. Abrahamu hakujua kama muda si mrefu kuna kitu kingetokea na kwamba angejaribiwa zaidi kuliko alivyokuwa akihofia. Ni kuhusu Isaka ambaye ndiye aliyebakia baada ya Ishmaieli kuondoka. Sikiliza vizuri ujifunze kupitia kipindi hiki.
5. Agano 3
Mungu anaweka Agano la kumpa uzao mwingi Abramu.
Mungu anamtokea Abramu na kuweka Agano naye. Agano la kumpa uzao kupitia mke wake Sarai. Mungu anamwambia "Sarai mke wako, hutamwita tena Sarai, bali kuanzia sasa utamwita Sara! Nitambariki, na atakuzalia mtoto wa kiume, naye atakuwa taifa, mataifa yatatoka kwake". Karibu kusikiliza kipindi hiki.
4. Agano 2
Ishmaeli anazaliwa na Hajiri mjakazi wa Sarai.
Katika Agano 2 ni jinsi Abramu alivyopata mtoto kupitia Hajiri. Malaika alimwambia Hajiri, "Ninataka kufanya uzao wako uwe mwingi kiasi kisichohesabika. Hajiri, Unangojea mtoto, na atakuwa mtoto wa kiume. Jina lake utamwita Ishmaeli". Yaani Mungu anasikia. Karibu kusikiliza.
3. AGANO 1
Safari ya Abramu kwenda nchi aliyoahidiwa na Mungu. Sehemu ya kwanza
Safari ya Abramu kwenda nchi aliyoahidiwa na Mungu ilikuwa ndefu yenye misukosuko na vikwazo vingi. Ilimchukuwa miaka kadhaa kufika nchi aliyoahidiwa na Mungu. Usiku mmoja Abramu alikuwa nje ya hema lake jangwani na kundi kubwa la watu aliofuatana nao kutoka vitani wakijenga hema kufanya makazi yao hapo. Abramu alitoka kwenye vita kuwakomboa ndugu zake. Alifanikiwa lakini alipata jeraha mguuni. Sikiliza kipindi hiki ujifunze mengi kuhusu Agano.