podcast, Michezo ya redio Cathbert Msemo podcast, Michezo ya redio Cathbert Msemo

7. Agano 5

Ibrahimu anapatwa na majaribu makubwa.

Urithi wa Adamu - Agano 5
Hammerson Luhanga na Roger Gihlemoen

Abrahamu aliumia sana kumfukuza Ishmaeli,kwani alimpenda kama mtoto wake na alimfurahia. Pia Ilikuwa aibu kubwa kumfukuza. Abrahamu hakujua kama muda si mrefu kuna kitu kingetokea na kwamba angejaribiwa zaidi kuliko alivyokuwa akihofia. Ni kuhusu Isaka ambaye ndiye aliyebakia baada ya Ishmaieli kuondoka. Sikiliza vizuri ujifunze kupitia kipindi hiki.

Agano_Radio_07.jpg



Read More
Michezo ya redio, podcast Cathbert Msemo Michezo ya redio, podcast Cathbert Msemo

5. Agano 3

Mungu anaweka Agano la kumpa uzao mwingi Abramu.

Urithi wa Adamu - Agano 3
Hammerson Luhanga na Roger Gihlemoen

Mungu anamtokea Abramu na kuweka Agano naye. Agano la kumpa uzao kupitia mke wake Sarai. Mungu anamwambia "Sarai mke wako, hutamwita tena Sarai, bali kuanzia sasa utamwita Sara! Nitambariki, na atakuzalia mtoto wa kiume, naye atakuwa taifa, mataifa yatatoka kwake". Karibu kusikiliza kipindi hiki.

Agano_Radio_05.jpg
Read More
Michezo ya redio, podcast Cathbert Msemo Michezo ya redio, podcast Cathbert Msemo

4. Agano 2

Ishmaeli anazaliwa na Hajiri mjakazi wa Sarai.

Urithi wa Adamu - Agano 2
Hammerson Luhanga na Roger Gihlemoen

Katika Agano 2 ni jinsi Abramu alivyopata mtoto kupitia Hajiri. Malaika alimwambia Hajiri, "Ninataka kufanya uzao wako uwe mwingi kiasi kisichohesabika. Hajiri, Unangojea mtoto, na atakuwa mtoto wa kiume. Jina lake utamwita Ishmaeli". Yaani Mungu anasikia. Karibu kusikiliza.

Agano_Radio_04.jpg
Read More
Michezo ya redio, podcast Cathbert Msemo Michezo ya redio, podcast Cathbert Msemo

3. AGANO 1

Safari ya Abramu kwenda nchi aliyoahidiwa na Mungu. Sehemu ya kwanza

Urithi wa Adamu - Agano 1
Hammerson Luhanga na Roger Gihlemoen

Safari ya Abramu kwenda nchi aliyoahidiwa na Mungu ilikuwa ndefu yenye misukosuko na vikwazo vingi. Ilimchukuwa miaka kadhaa kufika nchi aliyoahidiwa na Mungu. Usiku mmoja Abramu alikuwa nje ya hema lake jangwani na kundi kubwa la watu aliofuatana nao kutoka vitani wakijenga hema kufanya makazi yao hapo. Abramu alitoka kwenye vita kuwakomboa ndugu zake. Alifanikiwa lakini alipata jeraha mguuni. Sikiliza kipindi hiki ujifunze mengi kuhusu Agano.

Agano_Radio_03.jpg
Read More