Soma habari mpya kutoka Soma Biblia

Cathbert Msemo Cathbert Msemo

NDOA YENYE FURAHA

Usijinyime furaha ya kuwa na kitabu hiki kama msaidizi wako katika kazi uliyo nayo ya kufundisha mambo ya ndoa. Mwandishi mmoja wa Ndoa Yenye Furaha ni Askofu Blaston Gaville, KKKT Dayosisi ya Iringa, ambaye ana uzoefu mwingi wa kuwafundisha na kuwashauri wanandoa.

Read More
Magazeti, RIZIKI Cathbert Msemo Magazeti, RIZIKI Cathbert Msemo

RIZIKI TOLEO 4/2019 linapatikana "JE! YESU AMEPOTEA NJIA?"

Katika toleo hili la RIZIKI tunajadili kurudi kwa Yesu kama alivyoahidi. Lengo ni kusaidiana kama kanisa kupeana maarifa yenye uhakika juu ya kuja kwa Yesu mara ya pili. Malengo ni wazi: Kwanza, tuwe na mafundisho sahihi kuhusu kurudi kwa Yesu. Pili, tuepukane na mafundisho ya uongo kuhusu jambo hili. Na tatu, tusije tukakata tamaa kuwa Kristo harudi, kisha tukalegea katika kuitenda kazi ya Mungu. 

Read More
RIZIKI Cathbert Msemo RIZIKI Cathbert Msemo

RIZIKI TOLEO LA 1, 2019 - 'Ukristo ni utamaduni au imani?'

Katika toleo hili la RIZIKI tunachunguza kama Ukristo ni imani au utamaduni. Nia ni kukumbushana kuwa, mapokeo ya dini yanaweza kuwa mazoea au taratibu tupu zisizo na faida. Kama mwandishi mmoja alivyoandika, ndivyo taratibu zilivyo kama misingi yake haikujengwa katika Kristo. Lakini vilevile tamaduni na mapokeo zitafaa, tena zitakuwa na faida, kama zinatuelekeza kumwamini Yesu na kufanya mapenzi yake. Karibu usome toleo hili

Read More
Watoto na Vijana Cathbert Msemo Watoto na Vijana Cathbert Msemo

SIKU KUU YA MIKAELI NA WATOTO IMEKARIBIA

Ni furaha yetu kuona jinsi Kanisa linavyoweka siku kuu ya pekee kwa ajili ya watoto. Soma Biblia tunapenda kushiriki katika kazi ya kuwajenga watoto katika imani ya Kikristo kwa njia ya vitabu, Biblia na majarida kwa ajili ya watoto. Kwa hiyo tunatoa ofa maalum kwa sharika zote zinazopenda kuwapa watoto wao zawadi kwaajili ya siku kuu ya watoto.  

Read More
Magazeti Cathbert Msemo Magazeti Cathbert Msemo

Twende toleo no. 3, 2018 linapatikana sasa

Mpendwa msomaji wa Twende, uvumilivu ni tunda la Roho tunayepewa tunapomwamini Yesu. Biblia inatufundisha uvumilivu kupitia watu mbalimbali. Toleo hili limefafanua zaidi maana ya uvumilivu kwetu sisi Wakristo. Jipatie nakala yako kutoka Soma Biblia.

Read More
taarifa Anne Gihlemoen taarifa Anne Gihlemoen

TUMEJIFUNZA NA TUMEBURUDIKA - SEMINA YA WATUMISHI WA SOMA BIBLIA

Mwaka huu wafanyakazi wa Soma Biblia tulipata nafasi ya kukutana kwa pamoja katika kituo cha Mikutano cha Amabilis, mjini Morogoro kuanzia tarehe 23 hadi 27 Mei 2018. Wafanyakazi wa vituo vya Soma Biblia toka Arusha, Dar es salaam, Iringa, Mbeya na Mwanza walihudhuria semina hiyo. Pia tulikuwa na waendesha mada mbalimbali toka Chama cha Biblia Tanzania, na Mchg Oswald Ndelwa kutoka Iringa, ambaye aliendesha somo la Biblia kwa siku mbili. 

Read More